Matthew 24:32-35
32 a“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 33 bVivyo hivyo, myaonapo mambo haya yote, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni. 34 cAmin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia. 35 dMbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa
(Marko 13:32-37; Luka 17:26-30, 34-36)
Copyright information for
SwhKC